Daktari na Mwalimu
Daktari na Mwalimu
Daktari
Hii kazi ya Mwalimu, kweli haina thamani,
Ni kama mwendawazimu, kelele kutwa shuleni,
Na mimi
siheshimu, sitii maanani,
Kazi ya kujivunia, kweli ni ya Daktari.
Mwalimu
Ni wewe mwendawazimu, huna akili kichwani,
Wasema bila fahamu, hujui wasema nini,
Udokta hautimu,
bila kufika shuleni,
Kazi njema ya walimu, kutoa watu gizani.
Daktari
Kusoma hailazimu, mtu afike shuleni,
Kuna wengi mumu humu, wasomea barazani,
Na mengi wayafahamu, yaliyomo vitabuni,
Daktari ni muhimu, kwa kuokoa maisha.
Mwalimu
Hilo si maalumu, kuokoa maishani,
Tena unajidhulumu, waingia
kufuruni,
Hiyo kazi ya Karimu, ndiye
mwenye nusurani,
Kazi njema ya walimu, kutoa
watu gizani.
Daktari
Daktari ni muhimu, kukutoa
ujingani,
Mtu amekula sumu, maisha ya hatarini,
Budi atajilazimu, afike
kwangu nyumbani,
Daktari ni muhimu, kwa kuokoa
maisha.
Mwalimu
Asili ya binadamu, yatokana
na manani,
Narudi kutakalamu, nililosema
mwanzoni,
Asipopenda Karimu, bidiizo zifaeni?
Kazi njema ya walimu, kutoa
watu gizani.
Daktari
Hilo nalifahamu, silipingi abadani,
Amri ni ya Karimu, najua toka
zamani,
Japo mtu hana damu, asubiri kwa Manani,
Daktari ni muhimu, kwa kuokoa
maisha.
Mwalimu
Kidogo
natabasamu, na kicheko mdomoni,
Wa tele wendawazimu, moja ni wewe fulani,
Hivyo wale marehemu,
hawakwenda ugangani?
Kazi njema ya walimu, kutoa
watu gizani.
Daktari
Hilo mimi sikubali, nitafanya
nushindani,
Bora kuomba Jalali, si lazima
ugangani.
Unapopata ajali, mbona hukai nyumbani?
Daktari ni muhimu, kwa kuokoa
maisha.
Mwalimu
Hayo yako sikubali, na wala
siyaamini,
Tokea enzi azali, hako
Daktari nchini,
Watu hupata thakili, hutibiwa
majumbani,
Kazi njema ya walimu, kutoa
watu giza
Labels: ACADEMIC
1 Comments:
victor
Post a Comment
Subscribe to Post Comments [Atom]
<< Home